- Source #1
- View Source #1
- Source #2
- View Source #2
<div class="bbWrapper"></div>
- Tunachokijua
- Lamine Yamal ni mchezaji wa mpira wa miguu wa Hispania mwenye asili ya Morocco na Guinea Equatorial. Alizaliwa tarehe 13 Julai 2007. Yeye ni kijana mdogo ambaye ameonyesha vipaji vya hali ya juu na anaichezea klabu ya Barcelona katika ligi kuu ya Hispania, La Liga.
Picha ya Mchezaji kinda Lamine Yamal (17) akiwa amebeba mtoto (3) ikisambaa na kudaiwa kuwa ni mtoto wake imetumiwa kwenye mitandao mbalimbali tazama hapa na hapa
Moja wapo ya taarifa zinazosambaa kuhusu Lamine Yamal na mtoto aliyembeba
Ufuatiliaji wa JamiiCheck katika vyanzo mbalimbali umebaini kuwa taarifa inayodai mtoto huyo ni wa Yamal haina ukweli. JamiiCheck imebaini mtoto huyo aliyebebwa anaitwa Keyne Yamal ambaye ni mdogo wa Lamine na sio mtoto wake kama inavyodaiwa.
Taarifa inayoeleza uhusiano wa Lamine Yamal na Keyne Yamal
Endelea kutembelea Jukwaa la JamiiCheck ili kuwa karibu na taarifa zilizohakikiwa